Sunday, December 11, 2011

Mwenyekiti wa KIDO Mzee Ibrahimu Bigwomunda awahimiza waislamu kuleta watoto wao Kusoma Shule ya Sekondari ya KIDO karagwe Lubwera Kagenyi(Dec.2011)

Mwenyekiti wa KIDO Karagwe Mzee Ibrahimu Bigwomunda amesema tayari ameishapata walimu wenye Shahada za chuo kikuu kusimamia na kufundisha shule mpya ya sekondari ya KIDO wilayani Karagwe, amesema kuwa kwa uwezo wa Allah(SW) hatarajii kurudi nyuma katika kuhakikisha anaendeleza miradi ya KIDO akiwa na viongozi wa KIDO kwa ujumla. Uongozi wa KIDO karagwe umeisha muunga mkono katika hili kwani Primary ya KIDO Karagwe kwa sasa imeweza kuhitimisha watoto wa darasa la saba na wanategemea kujiunga kidato cha kwanza. Shule hizi za KIDO ni shule zinazofundisha masomo ya dini ya kiislamu kikamilifu na adabu njema za kiislamu na masomo ya kawaida ya kimazingira, kwa hiyo mtoto akitoka katika shule hizi za KIDO atakuwa amepata bahati ya kujua uislamu wake vizuri na dunia yake vizuri.
Shule zinatumia Lugha mbili za Kimataifa katika kufundisha yaani Kiarabu na Kiingereza

No comments:

Post a Comment

CHANGIA MAWAZO YAKO/USHAURI KWA MANUFAA YA JAMII. UNA MAWAZO YAKO NA YANAWEZA KUWA NA MANUFAA YATOE TAFADHALI. KARIBU SANA