Thursday, December 8, 2011

Akhlaq(Tabia) Njema Kwa mafundisho ya uislamu na Sheikh Musa Abeid Msikiti wa Kashai Markaz

Sheikh Musa ABEID Baada ya Swala ya Alfajiri alitoa nasaha kwa waislam kuhusu tabia njema za kiislam, aliongelea tabia nzuri na zenye kulinda heshima za muislam kama:

  1. Kutochana ndevu mbele ya watu
  2. Kutoshika shika ndevu mbele ya watu
  3. Kutochokonoa meno mbele ya watu
  4. Kutoweka vidole puani mbele ya watu
  5. Kutokata kucha mbele ya watu
  6. Kutosimamia watu waliokaa wakifanya mambo yao
  7. Kutolala ndani ya watu waliokaa
  8. Kutokaa bila kulala kati ya watu waliolala
  9. Kutonyoshea watu au mtu kidole akiwa mbali au karibu hata kama unamuongelea vizuri
  10. Kutolazimisha katika kuomba yaani kugagania kuomba
  11. Kutofanya urafiki na mtu muongo
  12. Kutojifanya rafiki wa tajiri asiyekusaidia lolote hata ukiwa na shida
  13. Kutokaa vijiweni au karibu na njia ila ukilazimika kukaa chunga haki zake kama kuinamisha macho, kuhamrisha mema na kuondoa maudhi kwa watu
  14. Kutotaniana na watoto na watu walioko chini yako kuzidi kiwango cha kawaida
  15. Kutorithisha mali zako na  bado uko hai:mfano: kugawa nyumba kwa mwanamke kuwa ni yake, mashamba, n.k
  16. Kutodhihirisha hali mbaya kiuchumi waziwazi kwa mwanamke wako bila ulazima wa kufanya hivyo.
  17. Kutofanya mali kuwa na thamani kuliko wewe. mfano: kuna watu wanafikia hatua kujidhalilisha ili wapate pesa kama waimbaji wakiwa uchi, michezo ya kuigiza(Comedy), Mashindano ya kuwania urembo, kumfanyia mpango haramu dada yako au shemeji yako, nk ili azini na mtu mwingine ili mradi umepewa mali, wanawake malaya ili wapate mali wanafanya zinaa kila muda na mtu yoyote.
  18. Kutotembea kwa magoti
Sheikh Musa Abeid amesema hii ni kuonyesha kuwa waislamu tuna muongozo kuhusu tabia njema katika kuishi na watu mbalimbali.
Si rahisi kupata mafunzo haya katika dini nyinginezo, hivyo tujitahidi kuzifanyia kazi kwa vitendo ili tuwe mfano wa kuigwa katika jamii. Insha Allah tujitahidi kusoma dini yetu na kuwafunza jamaa zetu uislam kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

CHANGIA MAWAZO YAKO/USHAURI KWA MANUFAA YA JAMII. UNA MAWAZO YAKO NA YANAWEZA KUWA NA MANUFAA YATOE TAFADHALI. KARIBU SANA