Thursday, August 9, 2012

Mafunzo ya uislam-Fiqh


FIQ-H A’QAAID

Mwenyezi  Mungu  Mtukufu 

1.  Mwenyezi  Mungu   Mtukufu  hajielezi  kwa  mtu  yoyote.
2.  Lazima  tukubali  Maamuzi  ya  Mwenyezi  Mungu  Mtukufu.
3.  Tusilalamike  na  matendo  ya  Mwenyezi  Mungu  Mtukufu.
4.  Mwenyezi  Mungu Mtukufu  anawapenda  walio  watiifu.
5.  Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  pekee  ndie  anae  jua  matukio  yatakayotokea  baadae.
6.  Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  pekee  ndie  anajua  wakati  gain  mtu  atazaliwa  na 
     Wakati  gani.atakufa.
7.  Mwenyezi  Mungu  Mtukufu pekee  ndie  anayeleta  mvua.
8.  Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  pekee  ndie  anaewaponesha  wagonjwa.
9.  Mwenyezi  Mungu  Mtikufu  ndie  anaebariki,  na  anawafanya  watu  kua  matajiri  au
     Maskini.
10. Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  pekee  ni  Mfalme  wa  wafalme  wote.
11. Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  pekee  ndie  mwingi  wa  kurehemu.
12. Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  ni  mwingi  wa  msamaha.
13. Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  ndie  anaempa  mtu  heshima  na  cheo.
14. Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  ni  msikivu  na  huona  kila  kitu.
15. Menyezi  Mungu  Mtukufu  pekee  ndie  anaefaidisha  au  anaweza  kumuathiri  mtu 
      Yoyote.
16. Mwenyezi  Mungu  Mtukufu  anatoa  muongozo  kwa  yule  anae  mtaka.
17.  Mwenyezi Mungu Mtukufu  anamwaga  rehma  zake  kwa  viumbe  vyake  vyote.
18.  Mwenyezi Mungu  Mtukufu  pekee  ndie  anae  toa  riziki.
19.  Tujaribu  kuzilinda  imani  zetu  na  tuishi  kutokana  na  mafundisho  ya  Mwenyezi 
      Mungu  Mtukufu  na  kipenzi  chake  mtune  Muhammad(s.a.w).

Kalimatut  Tawhiid

Laa  ilaaha  illa  llah wahdahu  laa  shariikalahu  lahul  mulku  walahul  hamdu  yuhyii  wayumiitu  biyadihilkhayru  wahuwa  a’laa kulli shay in qadiiru.

Tafsiri

Hapana  Mola  apasaye  kuabudiwa  kwa  haki ila   Allah   ni  mmoja  na  hana mshirika. Ufalme  ni  kwake na  sifa  zote  njema  ni  zakwake.  Anatoa maisha  na  anasababisha  kifo  katika  mikono  yake  yote  ni  mazuri  na  anauwezo  wa  kila  kitu.(Tir mithiy)

FIQ-H DINIYAAT

   HANAFIY
Kuna    faradh  ngapi  za  udhu?
(umoja  faradh, wingi  faraa-idh)

Kuna  faradh  nne  za  udhu.
Faradh  za  udhu ni:

  1. Kuosha  uso  wote  mara  moja.
  2. Kuosha   mikono  yote  mpaka   kwenye  vifundoni  mara  moja.
  3. Kupaka  maji  katika  kichwa  angalo  robo  mara  moja.
  4. Kuosha  miguu  yote  mpaka  kwenye  vifundo  mara  moja.

Jinsi  ya  kuweka  udhu.
  1. Elekea  qibla  wakati  wa  kuweka  udhu; baadae  weak  nia  ya  kuchukua  udhu.
  2. Soma:  Bismillahr  Rahmaanir Rahiim.
Kwa  jina  la  mwenyezi  Mungu,  Mwenye  kuneemesha  neema  kubwakubwa  na  Mwenye  kuneemesha  neema  ndogondogo.

      3.   Tumia  mswaki  na  baadae   osha  viganja  vyote viwili  mpaka  kwnye  vifundo 
             mara  tatu.  (Khilaal  ya  vidole  ifanywe   wakati  wa kuosha  mikono.mwanzoni
             mwa  kuweka  udhu.
   
 4.  Sukutua  mara  tatu  (tumia  mkono  wa  kulia).

  1. Weka  maji  kwenye  pua  na  safisha  tundu  za  pua  kwa  kutumia  kidole cha 
Kushoto  mara  tatu.

  1. Osha  uso  wote  mara  tatu.

7.   Eneo  la  uso  ni  kutoka  kwenye mstari  wa  nywele  juu  ya  paji  la  uso  mpaka
      chini  ya  kidevu,  na  kutoka kwenye  sikio  hadi  sikio jenjine.  Maji  lazima 
      yafike  kwenye  ngozi  ilioko  chini  ya  nyusi.

8.   Osha  mkono   wa  kulia  mpaka  kwenye  vifundo  vya juumara  tatu,  baadae 
     Osha  mkono wa kushoto mpaka  kwenye  vifundo  vya  juu  mara  tatu.

  1. Fanya  mas-h  ya  kichwa  chote, masikio, sehemu  ya  nyuma  ya  shingo, na 
Kufanya  khilaal  ya  ndevu  na  vidole  vya  mikono  yote.

  1. Baadae  osha  mguu  wa kulia  mpaka  kwenye  vifundo  mara  tatu; ukisha 
Osha  mguu  wa  kushoto  kwa  utaratibu  huo  huo  mara  tatu. (Khilaal  ya 
Vidole  vya  miguuni  ifantike mwanzoni  wakati  wa  kuosha  miguu).

  1. Baadae  fanya  khilaal  ya  vidole  vya  miguu.
  2. Soma  dua  baada  ya  kuchukua  udhu.



Maelezo  kwa   Ustaadh
      Wafahamishe  wanafunzi  kwamba  khilaal  ni  kupitisha  vidole  vyenye maji     vya  mkono  mmoja  hadi  vidole  vyenye  maji  vya  mkono  mwingine.  Khilaal  ya  ndevu  ni  kupitisha  vidole  vyenye  maji  vya  mikono  yote kwenye  ndevu   ikiwa  ikiwa  viganja  vyote  vikielekea  kwenye uso. Musha  na  khilaal  lazima  zielezwe  kwa  vitendo  na  waonyeshwe  wanafunzi.

Ni  yapi  majina  yaswala  tano  za  kila siku?


       
Faj-r         
Adhdhuh-r
Laa’swi-r
Maghrib
Ishaa’

Ni  yapi  majina  ya  miezi  ya  kiislam?

Majina  ya  miezi  ya  mwaka  ni:
1.      Muharram
2.      Safar
3.      Rabiul  Awwal
4.      Rabiul  Aakhir
5.      Jumadal  Uulaa
6.      Jumaadal  Aakhir
7.      Rajab
8.      Shaabaan
9.      Ramadhaan
10.  Shawwal
11.  DhulKaadah
12.  DhulHijja

E. FIQ-H:  AADAAB

Jinsi  Namna Gani  waislam  watumie  choo?

         1.Waislam  mwanzo  wasome  Bismillah  na  dua ya  kuingia  chooni.(Allahumma inniy audhubika minal ubuth wal abaith)
         2. Waislam  waingie  chooni  kwa  kuanzia  mguu  wa  kushoto  mwanzo.
         3. Waislam wasiingie  chooni  bila kuhifadhi  kichwa.
         4. Waislam  wasende  chooni  bila  viatu.
         5. Waislam  wasichuchumae  chooni  wakiwa  wameelekea  Qibla  na  wala  wasikae   wakiwa  migongo  yao  imeelekea  Qibla.
         6. Waislam  haatakiwi  kula, kunywa,  au  kuongea  chooni.
         7. Waislam  hawaruhusiwi  kusoma  vitabu  au  magazeti  chooni.
         8. Waislam hawaruhusiwi  kusoma  dua, kalmia au  aya  ya  Qur-aan chooni.
         9. Waislam   hawaruhusiwi kukojoa kwa  kusimama   sehemu  yoyote  hata kama  ni  chooni  au  ni sehemu  ya  kuogea.
       10. Waislam  hawaruhusiwi  kusimama  na  kukojoa  na  kukojoa  kwenye vichochoro  vya  majengo  au  nyumba, kwenye  ukuta, kwenye  vipango  na  mashimo juu  ya  miti, ,au  sehemu  ya  juu  au  kupingana  na  upepo.

      11. Mkojo  na  choo  kikubwa  ni  najisi  na  si  twahara. Hivi  si  twahara  wala  sio  safi  kutokana  na  Dini  yetu.  Mkojo na  choo  kikubwa  lazima  visafishwe na  ziondolewe  katika  mwili,  nguo, viatu  na  sehemu  tunazotumia  kwa  kuosha.  Hii  ifanyike  kwa  kutumia  maji  safi.

12. Kuosha  sehemu  za  siri  inapotokea  haja  ndogo  na  kubwa  inaitw  istinjaa.
13. Waislam  wafanye  istinjaa  kwa  kutumia  mkono  wa  kushoto, atumie maji  baada  ya  kukojoa  au  baada  ya  kujisaidia.
14. Waislam  watoke  nje  ya  choo  kwa  mguu  wa kulia.
15. Waislam  waoshe  mikono  yao  inapendeza  kwa  kutumia  sabuni,baada  ya  kutoka  chooni.
16. Waislam  wasijisaidie:

a)      Kwenye  mitaa  au  hadharani.
b)      Chini  ya  miti  ya  matunda.
c)      Miti  ambayo imeoteshwa  kwa  ajili  ya  kivuli  pembeni  mwa   barabara.
d)      Kwenye  bustani  za  binafsi  au  za  wote.
e)      Kwenye  mabawa  ya  kuogelea  au  mabawa  ya  maji.
f)        Sehemu  za  kuhifadhia  maji  au  sehemu  zinazomwagiliwa  maji.
g)      Pembeni  mwa  handaki  au  mto.

OFISI YETU

TUNA OFISI YA USHAURI NA TIBA DSM VINGUGUTI. UKIFIKA BUGURUNI SHEL SHUKA NA UPANDE MAGARI YA KWENDA VINGUGUTI , TELEMKA KITUO CHA POLISI KIITWACHO MTAKUJA. OFISI YETU IPO KARIBU NA NEW KINYUMA HOTEL.
UKIPANDA PIKIPIKI KUTOKA BUGURUNI SHEL NI SH 1,500/= TU KUFIKA OFISINI.

KWA MAELEZO ZAIDI TUMIA MAWASILIANO HAYA:

+255 752822056 ,+255654454398, +255 762219617

Email: tibaherbs@gmail.com

No comments:

Post a Comment

CHANGIA MAWAZO YAKO/USHAURI KWA MANUFAA YA JAMII. UNA MAWAZO YAKO NA YANAWEZA KUWA NA MANUFAA YATOE TAFADHALI. KARIBU SANA