Baada ya hapo kwa ufupi alitoa waadhi kuhusu funguo za mambo ya kheri ili waislamu wazijue hizo funguo na wazitumie kuelekea katika kheri Insha Allah.
Funguo katika mambo ya kheri ni hizi:
Ufunguo wa pepo ni Laa Illaha Illa llah
Ufunguo wa Riziq ni kuomba maghfirah na kujishughulisha kufanya kazi
Ufunguo wa kuongezewa na Allah ni kushukuru Allah
Ufunguo wa heshima ni Kumcha Allah na kufuata mafundisho ya Mtume(SAW)
Ufunguo wa Swala ni Twahara
Ufunguo wa Hija ni Kuhirimia nia ya Hija
Ufunguo wa taufiq ni hofu na shauku
Ufunguo wa Nusura ni subira
Pia Sheikh Musa Abed aligusia funguo katika mambo ya shari:
Ufunguo wa maovu ni pombe
Ufunguo wa zinaa ni mziki
Ufunguo wa udhalili ni uzembe
Ufunguo wa moto ni shirki
Ufunguo wa fitina ni uongo
No comments:
Post a Comment
CHANGIA MAWAZO YAKO/USHAURI KWA MANUFAA YA JAMII. UNA MAWAZO YAKO NA YANAWEZA KUWA NA MANUFAA YATOE TAFADHALI. KARIBU SANA