Friday, August 9, 2013

Sheikh Haruna Kichwabuta na Hotuba ya IDD Tarehe 9/8/2013

Bukoba IDD imesaliwa siku ya Tarehe 8/8/2013 na 9/8/2013 Hotuba ya Msikiti wa Ijumaa imesomwa na Sheikh wa Wilaya na pia yeye ni Kaimu Sheikh Mkuu-Bakwata Mkoa wa Kagera na ni Imamu Msikiti Bilele Bukoba Manispaa. Katika Hotuba hiyo amesisitiza mshikamano miongoni mwa waislam na Raia wa Tanzania kwa ujumla. Ameongelea kutogawanyika kwa mambo madogo miongoni mwa waumini.

Jana Sheikh Athumani alisoma Hotuba katika viwanja vya kashai Shule ya Msingi akisisitiza ucha Mungu na kujihesabu nafsi kabla ya mauti na kujitahidi kufanya mambo ya kheri na kuendelea kufanya hivyo hata baada ya funga ya mwezi wa Ramadhani. Ilifanyika harambee ya sekondari pale uwanjani ikiongozwa na Ustaz Faraji.